Friday, 8 March 2019

MRADI WA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI NA WAKISASA

Ukosekanaji wa Ajira nchini Tanzania ni miongoni mwa changamoto wanazokumbana nazo vijana wengi.Iwe ni wasomi au ambao huwapata nafasi ya kusonga mbele kielimu lakini wote hukumbwa na kukosekana kwa ajira.Kutokana na kuboreshwa kwa Sera ya Elimu nchini Tanzania imepelekea idadi ya vijana wengi kuhitimu elimu ya juu yaani Chuo Kikuu.Ongezeko la Vijana wanao maliza elimu ya juu imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka .Hivyo imepelekea kuwepo na ufinyu wa ajira za kuajiriwa kwa vijana.
Kuku ni miongoni mwa ndege wafugwao ambayo wanaweza kuchangia kupunguza ukosekanaji wa ajira kwa Vijana nchini.


MAHITAJI

  •  Kuku(tetea) 8 na Jogoo 1
  • Banda bora
  • Vyombo vya chakula na maji
  •    Chakula bora
  •   Madawa na chanjo kwajili ya magonjwa
  • Chanzo cha nishati joto na mwanga
  •  Elimu na ujuzi wa malezi bora
  •  Chombo au chumba cha kutunzia vifaranga
  •    Mayai ya kuku wa kisasa/mayai mabovu(ambayo hayakuanguliwa
  • Madaftari au kitabu cha kutunzia kumbukumbu
1  KUKU 8
..       Wakati wa kuanza mradi wako hakikisha una kuku 8 (matetea) wenye umri sawa na hawajawai kutaga hatamara moja. Chagua kuku wenye rangi nzuri kutoka katika familia bora kutegemea malengo ya mradi wako. Mfano kama lengo lako ni kuzalisha kuku wa kienyeji kwajili ya nyama basi chagua mbegu ambayo inakuwa haraka na yenye uzito mkubwa. Au ikiwa lengo ni mayai basi ni vema kuchagua aina ya kuku yenye kukua haraka na kutaga mayai mengi.
1    Ili kupunguza gharama za manunuzi ya kuku na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji ni vema kununua kuku wadogo ambao wametoka tu kuachishwa kulelewa na mama zao. Kuku hawa utawapata kwa bei ya chini, tena watafaa sana maana watakua na umri mmoja pia.
1  JOGOO 01


1    Jogoo mmoja tu anatosha kuwahudumia kuku matetea yote nane. Hakikisha katika uchaguzi wa jogoo bora lililochangamka, rangi mzuri, upanga umesimama, macho angavu, uzito wa kutosha, rangi nzuri na uwezo mkubwa wa kuzalisha. Ni vema mfugaji akaelewa kwamba kuku wote watakaozalishwa watategemea ubora wa jogoo wake. Uwezo wa kutaga kwa kuku na upatikanaji wa mayai pia hutegemea kwa karibu ubora wa jogoo aliyechaguliwa.


1    BANDA BORA
2.      Miongoni mwa mambo mhimu naya kwanza kuzingatiwa katika ufugaji wa kuku wa kienyeji kama mradi ni maandalizi ya banda bora. Kuku huhitaji banda bora ili wasiathirike na madhara mbalimbali. Mfugaji anatakiwa kuandaa banda lenye ukubwa wa mita 10 kwa mita 04. Yani urefu uwe mita 10 na upana upana wa mita 04. Kisha kata vyumba vya mita 2 urefu na upana mita 4 kutoka katika banda lako hivyo utakuwa na jumla ya vyumba vitano vyenye ukubwa unaolingana. Ujenzi uzingatie malighafi na vifaa vinavyopatikana kwa urahisi katika mazingira husika
      Baadhi ya vifaa hivyo ni kama ifuatavyo:-
§     Sakafu: Saruji, udongo, mbao, mianzi au fito
§     Kuta: Fito, mabanzi, mbao, nguzo mianzi,udongo, matofali, mawe, mabati na wavu
§     Paa: Nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati na vigae.
§     Wigo: Matofali, mbao, fito nguzo, mabanzi, mianzi, matete, wavu na mabati
    Banda bora la kuku linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-
§     Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama hatari.
§     Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika kwa urahisi.
§     Lijengwe sehemu yenye mwinuko isiyotuama maji, isiyo na upepo mkali na iwe mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu.
§     Liwe na vichanja kwa ajili ya kuku kupumzika na kulala.
§     Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji, kutagia, kuatamia na sehemu ya kulelea vifaranga.
§     Liwe na nafasi ya kutosha kulingana na idadi ya kuku na kuweka vyombo vya chakula na maji.

§     Kwenye mazingira ya joto banda liwe la ukuta mfupi na sehemu kubwa wazi yenye wavu hadi kufikia kwenye paa. Kwenye mazingira ya baridi banda liwe na ukuta mrefu unaokaribia paa na sehemu ndogo tu iwe wazi yenye wavu ili kupitisha hewa na mwanga.



1   USIKOSE MAKALA IJAYO TUTAJIFUNZA NAMNA YA UTUNZAJI WA VIFARANGA NA UANDAAJI WA CHAKULA CHA KUKU.....                                                          Ahsante  .

     

No comments:

Post a Comment